Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi

Sisi ni Nani

IJUE NHBRA

Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi ni Wakala ya Serikali iliyoanzishwa tarehe 1 septemba 2001. Wakala hii iko chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Ofisi zake ziko Mwenge barabara ya Sam Nujoma Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, umbali wa mita 400 kutoka barabara ya Ali Hassan Mwinyi.


KAZI ZA NHBRA

Kufanya utafiti kuhusu nyenzo za ujenzi na teknolojia ya ujenzi katika ngazi ya matumizi

Kushirikiana na Mamlaka za Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mashirika ya Kijamii, Wabia wa maendeleo na watu binafsi katika kuunda na kutoa mafunzo kwa /vikosi vya ujenzi wa nyumba na uzalishaj vyenzo katika ngazi ya wananchi.

Kuhamasisha kujenga uwezo (k.v kiufundi, kifedha na kiuongozi) wa watendaji wanaohusika na maswala ya nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Kuhakikisha kuwa mipango, sheria, kanuni za ujenzi, viwango na udhibiti vinalingana na uwezo, mahitaji, matakwa na matarajio ya sekta mbalimbali za wananchi

Kuhamasisha uzalishaji na matumizi ya vifaa vya ujenzi vya hapa nchini na vya gharama nafuu

Kuonyesha kwa vitendo matumizi ya vifaa vya ujenzi vya nchini

Kushauri serikali na wananchi mambo yanayohusu maswala ya maendeleo ya makazi


Office Location

Copyright © 2024 Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi Haki zote zimehifadhiwa. kanusho    MAKALA